1 |
WANAULIZANA nini? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078001.mp3
|
عَمَّ يَتَسَاءلُونَ |
2 |
Ile khabari kuu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078002.mp3
|
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ |
3 |
Ambayo kwayo wanakhitalifiana. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078003.mp3
|
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ |
4 |
La! Karibu watakuja jua. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078004.mp3
|
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ |
5 |
Tena la! Karibu watakuja jua. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078005.mp3
|
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ |
6 |
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078006.mp3
|
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا |
7 |
Na milima kama vigingi? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078007.mp3
|
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا |
8 |
Na tukakuumbeni kwa jozi? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078008.mp3
|
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا |
9 |
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078009.mp3
|
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا |
10 |
Na tukaufanya usiku ni nguo? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078010.mp3
|
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا |
11 |
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078011.mp3
|
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا |
12 |
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu? |
/content/ayah/audio/hudhaify/078012.mp3
|
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا |
13 |
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto; |
/content/ayah/audio/hudhaify/078013.mp3
|
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا |
14 |
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078014.mp3
|
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاء ثَجَّاجًا |
15 |
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078015.mp3
|
لِنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا |
16 |
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078016.mp3
|
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا |
17 |
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078017.mp3
|
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا |
18 |
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078018.mp3
|
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا |
19 |
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078019.mp3
|
وَفُتِحَتِ السَّمَاء فَكَانَتْ أَبْوَابًا |
20 |
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078020.mp3
|
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا |
21 |
Hakika Jahannamu inangojea! |
/content/ayah/audio/hudhaify/078021.mp3
|
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا |
22 |
Kwa walio asi ndio makaazi yao, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078022.mp3
|
لِلْطَّاغِينَ مَآبًا |
23 |
Wakae humo karne baada ya karne, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078023.mp3
|
لَابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا |
24 |
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078024.mp3
|
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا |
25 |
Ila maji yamoto sana na usaha, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078025.mp3
|
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا |
26 |
Ndio jaza muwafaka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078026.mp3
|
جَزَاء وِفَاقًا |
27 |
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078027.mp3
|
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا |
28 |
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078028.mp3
|
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا |
29 |
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078029.mp3
|
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا |
30 |
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu! |
/content/ayah/audio/hudhaify/078030.mp3
|
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا |
31 |
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078031.mp3
|
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا |
32 |
Mabustani na mizabibu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078032.mp3
|
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا |
33 |
Na wake walio lingana nao, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078033.mp3
|
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا |
34 |
Na bilauri zilizo jaa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/078034.mp3
|
وَكَأْسًا دِهَاقًا |
35 |
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo - |
/content/ayah/audio/hudhaify/078035.mp3
|
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا |
36 |
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078036.mp3
|
جَزَاء مِّن رَّبِّكَ عَطَاء حِسَابًا |
37 |
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake! |
/content/ayah/audio/hudhaify/078037.mp3
|
رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرحْمَنِ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا |
38 |
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078038.mp3
|
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرحْمَنُ وَقَالَ صَوَابًا |
39 |
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/078039.mp3
|
ذَلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ فَمَن شَاء اتَّخَذَ إِلَى رَبِّهِ مَآبًا |
40 |
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo! |
/content/ayah/audio/hudhaify/078040.mp3
|
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا |