1 |
Ya-Sin (Y. S.). |
/content/ayah/audio/hudhaify/036001.mp3
|
يس |
2 |
Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036002.mp3
|
وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ |
3 |
Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/036003.mp3
|
إِنَّكَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ |
4 |
Juu ya Njia Iliyo Nyooka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036004.mp3
|
عَلَى صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ |
5 |
Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036005.mp3
|
تَنزِيلَ الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ |
6 |
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036006.mp3
|
لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّا أُنذِرَ آبَاؤُهُمْ فَهُمْ غَافِلُونَ |
7 |
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036007.mp3
|
لَقَدْ حَقَّ الْقَوْلُ عَلَى أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ |
8 |
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036008.mp3
|
إِنَّا جَعَلْنَا فِي أَعْنَاقِهِمْ أَغْلاَلاً فَهِيَ إِلَى الأَذْقَانِ فَهُم مُّقْمَحُونَ |
9 |
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036009.mp3
|
وَجَعَلْنَا مِن بَيْنِ أَيْدِيهِمْ سَدًّا وَمِنْ خَلْفِهِمْ سَدًّا فَأَغْشَيْنَاهُمْ فَهُمْ لاَ يُبْصِرُونَ |
10 |
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036010.mp3
|
وَسَوَاء عَلَيْهِمْ أَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ لاَ يُؤْمِنُونَ |
11 |
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036011.mp3
|
إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ اتَّبَعَ الذِّكْرَ وَخَشِيَ الرَّحْمَن بِالْغَيْبِ فَبَشِّرْهُ بِمَغْفِرَةٍ وَأَجْرٍ كَرِيمٍ |
12 |
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036012.mp3
|
إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَى وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ وَكُلَّ شَيْءٍ أحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُبِينٍ |
13 |
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036013.mp3
|
وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلاً أَصْحَابَ الْقَرْيَةِ إِذْ جَاءهَا الْمُرْسَلُونَ |
14 |
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036014.mp3
|
إِذْ أَرْسَلْنَا إِلَيْهِمُ اثْنَيْنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزْنَا بِثَالِثٍ فَقَالُوا إِنَّا إِلَيْكُم مُّرْسَلُونَ |
15 |
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036015.mp3
|
قَالُوا مَا أَنتُمْ إِلاَّ بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَمَا أَنزَلَ الرَّحْمن مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلاَّ تَكْذِبُونَ |
16 |
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036016.mp3
|
قَالُوا رَبُّنَا يَعْلَمُ إِنَّا إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ |
17 |
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036017.mp3
|
وَمَا عَلَيْنَا إِلاَّ الْبَلاَغُ الْمُبِينُ |
18 |
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036018.mp3
|
قَالُوا إِنَّا تَطَيَّرْنَا بِكُمْ لَئِن لَّمْ تَنتَهُوا لَنَرْجُمَنَّكُمْ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ |
19 |
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036019.mp3
|
قَالُوا طَائِرُكُمْ مَعَكُمْ أَئِن ذُكِّرْتُم بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ مُّسْرِفُونَ |
20 |
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036020.mp3
|
وَجَاء مِنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَى قَالَ يَا قَوْمِ اتَّبِعُوا الْمُرْسَلِينَ |
21 |
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036021.mp3
|
اتَّبِعُوا مَن لاَّ يَسْأَلُكُمْ أَجْرًا وَهُم مُّهْتَدُونَ |
22 |
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036022.mp3
|
وَمَا لِي لاَ أَعْبُدُ الَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ |
23 |
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036023.mp3
|
أَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِ آلِهَةً إِن يُرِدْنِ الرَّحْمَن بِضُرٍّ لاَّ تُغْنِ عَنِّي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا وَلاَ يُنقِذُونِ |
24 |
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036024.mp3
|
إِنِّي إِذًا لَّفِي ضَلاَلٍ مُّبِينٍ |
25 |
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036025.mp3
|
إِنِّي آمَنتُ بِرَبِّكُمْ فَاسْمَعُونِ |
26 |
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua |
/content/ayah/audio/hudhaify/036026.mp3
|
قِيلَ ادْخُلِ الْجَنَّةَ قَالَ يَا لَيْتَ قَوْمِي يَعْلَمُونَ |
27 |
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036027.mp3
|
بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُكْرَمِينَ |
28 |
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036028.mp3
|
وَمَا أَنزَلْنَا عَلَى قَوْمِهِ مِن بَعْدِهِ مِنْ جُندٍ مِّنَ السَّمَاء وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ |
29 |
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036029.mp3
|
إِن كَانَتْ إِلاَّ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ خَامِدُونَ |
30 |
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036030.mp3
|
يَا حَسْرَةً عَلَى الْعِبَادِ مَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلاَّ كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُون |
31 |
Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036031.mp3
|
أَلَمْ يَرَوْا كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنْ الْقُرُونِ أَنَّهُمْ إِلَيْهِمْ لاَ يَرْجِعُونَ |
32 |
Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036032.mp3
|
وَإِن كُلٌّ لَّمَّا جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ |
33 |
Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036033.mp3
|
وَآيَةٌ لَّهُمُ الْأَرْضُ الْمَيْتَةُ أَحْيَيْنَاهَا وَأَخْرَجْنَا مِنْهَا حَبًّا فَمِنْهُ يَأْكُلُونَ |
34 |
Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake, |
/content/ayah/audio/hudhaify/036034.mp3
|
وَجَعَلْنَا فِيهَا جَنَّاتٍ مِن نَّخِيلٍ وَأَعْنَابٍ وَفَجَّرْنَا فِيهَا مِنْ الْعُيُونِ |
35 |
Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036035.mp3
|
لِيَأْكُلُوا مِن ثَمَرِهِ وَمَا عَمِلَتْهُ أَيْدِيهِمْ أَفَلَا يَشْكُرُونَ |
36 |
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036036.mp3
|
سُبْحَانَ الَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّهَا مِمَّا تُنبِتُ الْأَرْضُ وَمِنْ أَنفُسِهِمْ وَمِمَّا لَا يَعْلَمُونَ |
37 |
Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036037.mp3
|
وَآيَةٌ لَّهُمْ اللَّيْلُ نَسْلَخُ مِنْهُ النَّهَارَ فَإِذَا هُم مُّظْلِمُونَ |
38 |
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036038.mp3
|
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ذَلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ |
39 |
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036039.mp3
|
وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّى عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ |
40 |
Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036040.mp3
|
لَا الشَّمْسُ يَنبَغِي لَهَا أَن تُدْرِكَ الْقَمَرَ وَلَا اللَّيْلُ سَابِقُ النَّهَارِ وَكُلٌّ فِي فَلَكٍ يَسْبَحُونَ |
41 |
Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036041.mp3
|
وَآيَةٌ لَّهُمْ أَنَّا حَمَلْنَا ذُرِّيَّتَهُمْ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ |
42 |
Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036042.mp3
|
وَخَلَقْنَا لَهُم مِّن مِّثْلِهِ مَا يَرْكَبُونَ |
43 |
Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/036043.mp3
|
وَإِن نَّشَأْ نُغْرِقْهُمْ فَلَا صَرِيخَ لَهُمْ وَلَا هُمْ يُنقَذُونَ |
44 |
Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036044.mp3
|
إِلَّا رَحْمَةً مِّنَّا وَمَتَاعًا إِلَى حِينٍ |
45 |
Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa... |
/content/ayah/audio/hudhaify/036045.mp3
|
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّقُوا مَا بَيْنَ أَيْدِيكُمْ وَمَا خَلْفَكُمْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ |
46 |
Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036046.mp3
|
وَمَا تَأْتِيهِم مِّنْ آيَةٍ مِّنْ آيَاتِ رَبِّهِمْ إِلَّا كَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ |
47 |
Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036047.mp3
|
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ أَنفِقُوا مِمَّا رَزَقَكُمْ اللَّهُ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَنُطْعِمُ مَن لَّوْ يَشَاء اللَّهُ أَطْعَمَهُ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ |
48 |
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036048.mp3
|
وَيَقُولُونَ مَتَى هَذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ |
49 |
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036049.mp3
|
مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً تَأْخُذُهُمْ وَهُمْ يَخِصِّمُونَ |
50 |
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036050.mp3
|
فَلَا يَسْتَطِيعُونَ تَوْصِيَةً وَلَا إِلَى أَهْلِهِمْ يَرْجِعُونَ |
51 |
Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036051.mp3
|
وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَى رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ |
52 |
Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036052.mp3
|
قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا هَذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ |
53 |
Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036053.mp3
|
إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ |
54 |
Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036054.mp3
|
فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ |
55 |
Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036055.mp3
|
إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ |
56 |
Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036056.mp3
|
هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِؤُونَ |
57 |
Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036057.mp3
|
لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ |
58 |
"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036058.mp3
|
سَلَامٌ قَوْلًا مِن رَّبٍّ رَّحِيمٍ |
59 |
Na enyi wakosefu! Jitengeni leo! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036059.mp3
|
وَامْتَازُوا الْيَوْمَ أَيُّهَا الْمُجْرِمُونَ |
60 |
Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036060.mp3
|
أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَا بَنِي آدَمَ أَن لَّا تَعْبُدُوا الشَّيْطَانَ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ |
61 |
Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036061.mp3
|
وَأَنْ اعْبُدُونِي هَذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ |
62 |
Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036062.mp3
|
وَلَقَدْ أَضَلَّ مِنكُمْ جِبِلًّا كَثِيراً أَفَلَمْ تَكُونُوا تَعْقِلُونَ |
63 |
Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036063.mp3
|
هَذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ |
64 |
Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036064.mp3
|
اصْلَوْهَا الْيَوْمَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ |
65 |
Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036065.mp3
|
الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ |
66 |
Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036066.mp3
|
وَلَوْ نَشَاء لَطَمَسْنَا عَلَى أَعْيُنِهِمْ فَاسْتَبَقُوا الصِّرَاطَ فَأَنَّى يُبْصِرُونَ |
67 |
Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036067.mp3
|
وَلَوْ نَشَاء لَمَسَخْنَاهُمْ عَلَى مَكَانَتِهِمْ فَمَا اسْتَطَاعُوا مُضِيًّا وَلَا يَرْجِعُونَ |
68 |
Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036068.mp3
|
وَمَنْ نُعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِي الْخَلْقِ أَفَلَا يَعْقِلُونَ |
69 |
Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036069.mp3
|
وَمَا عَلَّمْنَاهُ الشِّعْرَ وَمَا يَنبَغِي لَهُ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْآنٌ مُّبِينٌ |
70 |
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036070.mp3
|
لِيُنذِرَ مَن كَانَ حَيًّا وَيَحِقَّ الْقَوْلُ عَلَى الْكَافِرِينَ |
71 |
Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036071.mp3
|
أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا خَلَقْنَا لَهُمْ مِمَّا عَمِلَتْ أَيْدِينَا أَنْعَامًا فَهُمْ لَهَا مَالِكُونَ |
72 |
Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036072.mp3
|
وَذَلَّلْنَاهَا لَهُمْ فَمِنْهَا رَكُوبُهُمْ وَمِنْهَا يَأْكُلُونَ |
73 |
Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036073.mp3
|
وَلَهُمْ فِيهَا مَنَافِعُ وَمَشَارِبُ أَفَلَا يَشْكُرُونَ |
74 |
Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036074.mp3
|
وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّهِ آلِهَةً لَعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ |
75 |
Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036075.mp3
|
لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُندٌ مُّحْضَرُونَ |
76 |
Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036076.mp3
|
فَلَا يَحْزُنكَ قَوْلُهُمْ إِنَّا نَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ |
77 |
Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri! |
/content/ayah/audio/hudhaify/036077.mp3
|
أَوَلَمْ يَرَ الْإِنسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِن نُّطْفَةٍ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٌ مُّبِينٌ |
78 |
Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika? |
/content/ayah/audio/hudhaify/036078.mp3
|
وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِيَ خَلْقَهُ قَالَ مَنْ يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ |
79 |
Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036079.mp3
|
قُلْ يُحْيِيهَا الَّذِي أَنشَأَهَا أَوَّلَ مَرَّةٍ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ |
80 |
Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036080.mp3
|
الَّذِي جَعَلَ لَكُم مِّنَ الشَّجَرِ الْأَخْضَرِ نَارًا فَإِذَا أَنتُم مِّنْهُ تُوقِدُونَ |
81 |
Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036081.mp3
|
أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَى أَنْ يَخْلُقَ مِثْلَهُم بَلَى وَهُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ |
82 |
Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036082.mp3
|
إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَنْ يَقُولَ لَهُ كُنْ فَيَكُونُ |
83 |
Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/036083.mp3
|
فَسُبْحَانَ الَّذِي بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ |