1 |
Litakapo tukia hilo Tukio |
/content/ayah/audio/hudhaify/056001.mp3
|
إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ |
2 |
Hapana cha kukanusha kutukia kwake. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056002.mp3
|
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ |
3 |
Literemshalo linyanyualo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056003.mp3
|
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ |
4 |
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056004.mp3
|
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا |
5 |
Na milima itapo sagwasagwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056005.mp3
|
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا |
6 |
Iwe mavumbi yanayo peperushwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056006.mp3
|
فَكَانَتْ هَبَاء مُّنبَثًّا |
7 |
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:- |
/content/ayah/audio/hudhaify/056007.mp3
|
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً |
8 |
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056008.mp3
|
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ |
9 |
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056009.mp3
|
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ |
10 |
Na wa mbele watakuwa mbele. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056010.mp3
|
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ |
11 |
Hao ndio watakao karibishwa |
/content/ayah/audio/hudhaify/056011.mp3
|
أُوْلَئِكَ الْمُقَرَّبُونَ |
12 |
Katika Bustani zenye neema. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056012.mp3
|
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ |
13 |
Fungu kubwa katika wa mwanzo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056013.mp3
|
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ |
14 |
Na wachache katika wa mwisho. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056014.mp3
|
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ |
15 |
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056015.mp3
|
عَلَى سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ |
16 |
Wakiviegemea wakielekeana. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056016.mp3
|
مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ |
17 |
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056017.mp3
|
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ |
18 |
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056018.mp3
|
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ |
19 |
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056019.mp3
|
لَا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ |
20 |
Na matunda wayapendayo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056020.mp3
|
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ |
21 |
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056021.mp3
|
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ |
22 |
Na Mahurulaini, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056022.mp3
|
وَحُورٌ عِينٌ |
23 |
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056023.mp3
|
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ |
24 |
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056024.mp3
|
جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ |
25 |
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056025.mp3
|
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا |
26 |
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056026.mp3
|
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا |
27 |
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056027.mp3
|
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ |
28 |
Katika mikunazi isiyo na miba, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056028.mp3
|
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ |
29 |
Na migomba iliyo pangiliwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056029.mp3
|
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ |
30 |
Na kivuli kilicho tanda, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056030.mp3
|
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ |
31 |
Na maji yanayo miminika, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056031.mp3
|
وَمَاء مَّسْكُوبٍ |
32 |
Na matunda mengi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056032.mp3
|
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ |
33 |
Hayatindikii wala hayakatazwi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056033.mp3
|
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ |
34 |
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056034.mp3
|
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ |
35 |
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056035.mp3
|
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاء |
36 |
Na tutawafanya vijana, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056036.mp3
|
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا |
37 |
Wanapendana na waume zao, hirimu moja. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056037.mp3
|
عُرُبًا أَتْرَابًا |
38 |
Kwa ajili ya watu wa kuliani. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056038.mp3
|
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ |
39 |
Fungu kubwa katika wa mwanzo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056039.mp3
|
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ |
40 |
Na fungu kubwa katika wa mwisho. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056040.mp3
|
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ |
41 |
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056041.mp3
|
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ |
42 |
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056042.mp3
|
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ |
43 |
Na kivuli cha moshi mweusi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056043.mp3
|
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ |
44 |
Si cha kuburudisha wala kustarehesha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056044.mp3
|
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ |
45 |
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056045.mp3
|
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُتْرَفِينَ |
46 |
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056046.mp3
|
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ |
47 |
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056047.mp3
|
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَئِنَّا لَمَبْعُوثُونَ |
48 |
Au baba zetu wa zamani? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056048.mp3
|
أَوَ آبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ |
49 |
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho |
/content/ayah/audio/hudhaify/056049.mp3
|
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ |
50 |
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056050.mp3
|
لَمَجْمُوعُونَ إِلَى مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ |
51 |
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056051.mp3
|
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ |
52 |
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056052.mp3
|
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ |
53 |
Na kwa mti huo mtajaza matumbo. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056053.mp3
|
فَمَالِؤُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ |
54 |
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056054.mp3
|
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ |
55 |
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056055.mp3
|
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ |
56 |
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056056.mp3
|
هَذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ |
57 |
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056057.mp3
|
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ |
58 |
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056058.mp3
|
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ |
59 |
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056059.mp3
|
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ |
60 |
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi |
/content/ayah/audio/hudhaify/056060.mp3
|
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ |
61 |
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056061.mp3
|
عَلَى أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ |
62 |
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056062.mp3
|
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَى فَلَوْلَا تَذكَّرُونَ |
63 |
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056063.mp3
|
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ |
64 |
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056064.mp3
|
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ |
65 |
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056065.mp3
|
لَوْ نَشَاء لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ |
66 |
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika; |
/content/ayah/audio/hudhaify/056066.mp3
|
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ |
67 |
Bali sisi tumenyimwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056067.mp3
|
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ |
68 |
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056068.mp3
|
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاء الَّذِي تَشْرَبُونَ |
69 |
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056069.mp3
|
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ |
70 |
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056070.mp3
|
لَوْ نَشَاء جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ |
71 |
Je! Mnauona moto mnao uwasha? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056071.mp3
|
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ |
72 |
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056072.mp3
|
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِؤُونَ |
73 |
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056073.mp3
|
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ |
74 |
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056074.mp3
|
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ |
75 |
Basi naapa kwa maanguko ya nyota, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056075.mp3
|
فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ |
76 |
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua! |
/content/ayah/audio/hudhaify/056076.mp3
|
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ |
77 |
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056077.mp3
|
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ |
78 |
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056078.mp3
|
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ |
79 |
Hapana akigusaye ila walio takaswa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056079.mp3
|
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ |
80 |
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056080.mp3
|
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ |
81 |
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056081.mp3
|
أَفَبِهَذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ |
82 |
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056082.mp3
|
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ |
83 |
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056083.mp3
|
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ |
84 |
Na nyinyi wakati huo mnatazama! |
/content/ayah/audio/hudhaify/056084.mp3
|
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ |
85 |
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056085.mp3
|
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَكِن لَّا تُبْصِرُونَ |
86 |
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056086.mp3
|
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ |
87 |
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? |
/content/ayah/audio/hudhaify/056087.mp3
|
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ |
88 |
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056088.mp3
|
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ |
89 |
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056089.mp3
|
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّةُ نَعِيمٍ |
90 |
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056090.mp3
|
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ أَصْحَابِ الْيَمِينِ |
91 |
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056091.mp3
|
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ |
92 |
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056092.mp3
|
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ |
93 |
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, |
/content/ayah/audio/hudhaify/056093.mp3
|
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ |
94 |
Na kutiwa Motoni. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056094.mp3
|
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ |
95 |
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056095.mp3
|
إِنَّ هَذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ |
96 |
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. |
/content/ayah/audio/hudhaify/056096.mp3
|
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ |