| 1 |
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075001.mp3
|
لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ |
| 2 |
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075002.mp3
|
وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ |
| 3 |
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075003.mp3
|
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَجْمَعَ عِظَامَهُ |
| 4 |
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075004.mp3
|
بَلَى قَادِرِينَ عَلَى أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ |
| 5 |
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075005.mp3
|
بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ |
| 6 |
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075006.mp3
|
يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ |
| 7 |
Basi jicho litapo dawaa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075007.mp3
|
فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ |
| 8 |
Na mwezi utapo patwa, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075008.mp3
|
وَخَسَفَ الْقَمَرُ |
| 9 |
Na likakusanywa jua na mwezi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075009.mp3
|
وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ |
| 10 |
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075010.mp3
|
يَقُولُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ |
| 11 |
La! Hapana pa kukimbilia! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075011.mp3
|
كَلَّا لَا وَزَرَ |
| 12 |
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075012.mp3
|
إِلَى رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ |
| 13 |
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075013.mp3
|
يُنَبَّأُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ |
| 14 |
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075014.mp3
|
بَلِ الْإِنسَانُ عَلَى نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ |
| 15 |
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075015.mp3
|
وَلَوْ أَلْقَى مَعَاذِيرَهُ |
| 16 |
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075016.mp3
|
لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ |
| 17 |
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075017.mp3
|
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ |
| 18 |
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075018.mp3
|
فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ |
| 19 |
Kisha ni juu yetu kuubainisha. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075019.mp3
|
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ |
| 20 |
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075020.mp3
|
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ |
| 21 |
Na mnaacha maisha ya Akhera. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075021.mp3
|
وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ |
| 22 |
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075022.mp3
|
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ |
| 23 |
Zinamwangallia Mola wao Mlezi. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075023.mp3
|
إِلَى رَبِّهَا نَاظِرَةٌ |
| 24 |
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075024.mp3
|
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ |
| 25 |
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075025.mp3
|
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ |
| 26 |
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075026.mp3
|
كَلَّا إِذَا بَلَغَتْ التَّرَاقِيَ |
| 27 |
Na pakasemwa: Nani wa kumganga? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075027.mp3
|
وَقِيلَ مَنْ رَاقٍ |
| 28 |
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki; |
/content/ayah/audio/hudhaify/075028.mp3
|
وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ |
| 29 |
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi, |
/content/ayah/audio/hudhaify/075029.mp3
|
وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ |
| 30 |
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075030.mp3
|
إِلَى رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ |
| 31 |
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075031.mp3
|
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّى |
| 32 |
Bali alikanusha, na akageuka. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075032.mp3
|
وَلَكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّى |
| 33 |
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075033.mp3
|
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَى أَهْلِهِ يَتَمَطَّى |
| 34 |
Ole wako, ole wako! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075034.mp3
|
أَوْلَى لَكَ فَأَوْلَى |
| 35 |
Kisha Ole wako, ole wako! |
/content/ayah/audio/hudhaify/075035.mp3
|
ثُمَّ أَوْلَى لَكَ فَأَوْلَى |
| 36 |
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075036.mp3
|
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى |
| 37 |
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075037.mp3
|
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَى |
| 38 |
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075038.mp3
|
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّى |
| 39 |
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke. |
/content/ayah/audio/hudhaify/075039.mp3
|
فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَى |
| 40 |
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu? |
/content/ayah/audio/hudhaify/075040.mp3
|
أَلَيْسَ ذَلِكَ بِقَادِرٍ عَلَى أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَى |